Yalipowashika, magonjwa na njaa, na umasikini
Mukahangaika, kwa zenu fadhaa, kusaka auni
Mukatawanyika, kukimbia baa, kwenda ugenini
Mukamiminika, mote kasambaa, kote mabarani
Nako kapokewa
Mukaauniwa
Mwengine mukawa, kwa yenu khiyana, munamukoloni